BY APOSTLE SHADRACK
LUHWAGO
0764444277 or 0712105099
BWANA YESU
APEWE UTUKUFU, TAIFA TEULE LA MUNGU
Ninayo furaha kubwa siku ya leo kukuletea ujumbe huu
ambao utakuwa chemichemi ya kufahamu makao yako ya milele, na namna ikupasavyo
kutenda angali u hai hapa duniani
Ndugu zangu katika KRISTO YESU neema ya Bwana wetu
Yesu Kristo na ushirika wa Roho mtakatifu uwe nasi sote, kwa maana sisi hapa
duniani Tu wapitaji/ wasafiri. Na imetupasa kuishi na kuenenda kama
msafiri.
Kwa maana Msafiri hujua wapi anakwenda!!!!! Msafiri huchagua usafiri gani atumie ili
afike sawasawa na anavyotarajia kufika ikitegemea umbali wa wapi
anakwenda!!!!!! Msafiri hawezi kutumia
punda au trekta kusafiri kutoka Tanzania kwenda marekani ,kwa sababu punda au
trekta haviwezi kupita kwenye maji.
Ndivyo ilivyo kwa sisi wana wa Mungu tuliopo hapa
duniani , kwa maana aina ya Maisha, matendo , maneno na kuketi kwetu ndiyo
chombo cha kusafiria kufika kwenye makao ya umilele. Ifahamike kuwa wanadamu
imetupasa kujua kuwa KUNA MAISHA MENGINE baada ya MAISHA HAYA . na MAISHA HAYA yaani ya hapa duniani
yamefungwa na MUDA angali MAISHA YALE
MENGINE yamefungwa na UMILELE. Umilele huo yaweza kuwa MOTONI AU MBINGUNI(YERUSALEMU).
Imeandikwa katika kitabu cha 1
petro 2:11 – 12 kuwa ‘’ English:
Beloved, I exhort YOU as aliens and
temporary residents to keep abstaining from fleshly desires, which are the very
ones that carry on a conflict against the soul.
Swahili:
“Wapenzi, nawasihi kama wapitaji na wasafiri,
ziepukeni tamaa za mwili zipiganazo na roho”
Neno KUSIHI ni Zaidi ya kuomba ,lenye maana ya
kusisitiza, na maandiko haya yanasema KUISHI KAMA MPITAJI NA MSAFIRI. Ipo siku
itakapofika ambapo watu wataomboleza ya kwamba umeondoka yaani umekufa ,akina
mama na watoto watalia machozi kwa
uchungu wakikumbuka fadhila zako kwao lakini wewe kumbuka utaingia either
MOTONI AU MBINGUNI kwa kadri ya matendo yako ya hapa duniani. Kwa version ya
kiingereza imeandikwa “ AS ALIENS AND TEMPORALY RESIDENTS) . watu wengi
tumejisahau ya kwamba sisi hapa duniani tunapita. Tumekuwa tukiishi kwa mazoea
, tukiamka na kula kama watu tuliofika tayari , kana kwamba tutaishi hapa
duniani milele.
Kumbuka kuwa “ mtu ni NAFSI na roho anayeishi ndani ya
nyumba” na nyumba hiyo ni MWILI, ipo siku mtu atatoka ndani ya nyumba hiyo na
kurudi kwake kwenye makao ya umilele , either MOTONI AU MBINGUNI.
Wapendwa katika Kristo Yesu, moto wa milele upo, na si
nadharia kwamba ni maagizo, JEHANAMU ipo , na inasubiri siku ya hukumu watu
wote waliotenda maovu waingizwe humo pamoja na yule ibilisi shetani.
Imetupasa kujitengezea Maisha ya utakatifu angali bado
wazima hapa duniani, bila kutafutiwa au kuombewa na wenzetu, kwani yule mwizi
pale msalabani alijiombea mwenyewe kwa Yesu, na pia mfalme DAUD katika uhai wake alijiombea mwenyewe,
Imeandikwa katika ZABURI 39: 1-12 English: 4"Jehovah,
please make me to know my end. What is the extent of my days? Let me know how
temporary (frail) (destitute) I am”.
Swahili: “Bwana, unijulishe mwisho
wangu, Na kiasi cha siku zangu ni kiasi gani; Nijue jinsi nilivyo dhaifu”.
MFALME DAUD ANAJIOMBEA MWENYEWE KWA
MUNGU ajulishwe mwisho wake kabla hajafa ili ajue alivyo mdhaifu na namna impasavyo
kutenda. Hivyo mimi na wewe tuandae Maisha yetu kabla hatujafa kwani hakuna nafasi
hata ya sekunde moja ya kuomba toba au rehema ukisha kufa. Hata wakikusindikiza
kwa maombi ya ki-BISHOP au kwa sala maalumu , ninakwambia leo hayatakusaidia. Nafasi
unayo leo ya kutafuta wokovu wa kweli utakaokufanya uwe na kibali siku ya
mwisho kwa ajili ya makao ya milele.
Imeandikwa katika kitabu cha DANIEL
12:1-3 1 Wakati huo
Mikaeli atasimama, jemadari mkuu, asimamaye upande wa wana wa watu wako; na
kutakuwa na wakati wa taabu, mfano wake haukuwapo tangu lilipoanza kuwapo taifa
hata wakati uo huo; na wakati huo watu wako wataokolewa; kila mmoja
atakayeonekana ameandikwa katika kitabu kile. 2 Tena, wengi wa hao walalao katika mavumbi ya nchi
wataamka, wengine wapate uzima wa milele, wengine aibu na kudharauliwa milele. 3 Na walio na hekima
watang'aa kama mwangaza wa anga; na hao waongozao wengi kutenda haki watang'aa
kama nyota milele na milele.
Kwa maana wanadamu waondokao katika
dunia hii HAWAFI bali WANA LALA ndivyo itakavyokuwa siku ya mwisho kwa ajili ya
Maisha ya UMILELE, miili ya watakatifu iliyolala chini ya ardhi itafufuliwa kwa
shangwe na furaha na kuingia mbinguni, wakati miili ya wale waovu itaingia
motoni kuunguzwa milele pamoja na shetani.
Imeandikwa katika kitabu cha UFUNUO
WA YOHANA 20: 11- 15, 11 Kisha nikaona kiti cha enzi, kikubwa, cheupe, na yeye aketiye juu
yake; ambaye nchi na mbingu zikakimbia uso wake, na mahali pao hapakuonekana.
12 Nikawaona wafu,
wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu
vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao
wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa
na matendo yao. 13 Bahari ikawatoa wafu waliokuwamo ndani
yake; na Mauti na Kuzimu zikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake. Wakahukumiwa
kila mtu kwa kadiri ya matendo yake.14 Mauti
na Kuzimu zikatupwa katika lile ziwa la moto. Hii ndiyo mauti ya pili, yaani,
hilo ziwa la moto.15 Na iwapo mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha
uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto.
Ninahuzuni kubwa kutamka
kuwa watu wengi hawataingia mbinguni, kwa maana maovu yameongezeka, uzizi ,
uchawi, ugovi, usengenyaji, kuabudu miungu mingine , ibada za sanamu , watu
wamekuwa ni wapenda pesa na mali kuliko MUNGU, chuki zimeongezeka kila mahali,
nasema pole kwa wewe unayetenda haya , kwa maana huwezi kumuona MUNGU siku hiyo
na wala hutaingia mbinguni,
Maombi yangu ya leo
kwako mwanadamu ambaye bado una nafasi ya kumjua na kumtafuta MUNGU aliye hai
katika KRISTO YESU, ni kwamba geuka na umtumikie MUNGU kwa moyo wako wote na
kwa roho yako yote na kwa nguvu zako zote, na ndipo litapotimia neno
lililoandikwa katika kitabu cha MATENDO YA MITUME 13: 36 ya kwamba English:
"After David served his own generation by doing the will of
God, DID FELL ASLEEP with his fathers. His body decayed”. Swahili:
“Kwa maana Daudi, akiisha kulitumikia shauri la Mungu katika kizazi
chake, alilala, akawekwa pamoja na baba zake, akaona uharibifu”.
MUNGU AKUBARIKI NA
KUKUJAZIA NEEMA KWA SAFARI YAKO YA HAPA DUNIANI, KATIKA KRISTO YESU MWANA WA
MUNGU ALIYE HAI
AMEN.
No comments:
Post a Comment