SOMO: KIFO SIYO TUKIO BALI NI ROHO
Na apostle of JESUS CHRIST shadrack
luhwago , luhwagoshadrack17@gmail.com
0764444277/0712105099, www.lshadrackc.blogspot.com
@naihubiri injili kwa
kasi ya 4G@
BWANA
YESU APEWE SIFA TAIFA TEULE LA MUNGU………………………
NINAWASALIMU
WOTE KATIKA JINA LA YESU KRISTO..
ROHO
YA MUNGU YU PAMOJA NAMI KATIKA KUKULETEA SOMO HILI LA
LEO YA KWAMBA KIFO SIYO TUKIO BALI NI ROHO.
Kwanza
Tuombe : BABA KATIKA JINA LA YESU KRISTO asante kwa kutupa muda na wakati huu
ili tuweze kuelewa sisi waja wako yale uliyokusudia kutupa siku ya leo,
ninakushukuru ewe muumba wa mbingu na nchi kwa uhai, mafanikio, na afya njema
unayoendelea kutujalia, tunalitukuza jina lako kristo kwa rehema na neema
unayoimimina kwenye maisha yetu,nasi twashuhudia ushindi katika vita, uponyaji
na wokovu kwa jina lako kristo. ewe emanuel MUNGU pamoja na wanadamu, emanuel
pamoja na huyu kijana na mzee, emanuel pamoja na kusanyiko hili, emanuel pamoja
na wagonjwa wote ninakusihi uturehemu maana tumekutenda dhambi, nasi
twaitazamia damu ya kristo itupayo ukamilifu katika yote. aachilia ROHO WAKO
MTAKATIFU akafundishe haya uliyokusudia kwa waja wako huku ukimtumia mtumishi
wako kama chombo, kwa mamlaka niliyopewa na kristo ninamfunga yule adui shetani
katika anga, ardhi na maji kote namimina
damu ya kristo na kukabidhi himaya nzima ilindwe na malaika MIKAEL, GABRIEL NA RAFAEL. ni
katika jina la YESU KRISTO tunaomba kwa
kushukuru na kuamini , na kila mwenye pumzi aseme ameeen.
WAPENDWA
KATIKA KRISTO NAWASALIMU TENA KATIKA PENDO LA MUNGU WETU WA MBINGUNI
SIKU
YA LEO NIMETUMWA NA MUNGU KUONGEA NANYI NA KUWALETEENI UJUMBE KWAMBA KIFO
SIYO TUKIO BALI NI ROHO, nimatumaini
yangu kwamba uelewe kwa kiwango ambacho MUNGU amekusudia upate katika nyakati
za maisha ya kizazi cha sasa .
Nini
maana ya kifo?
Ni
mwisho wa maisha ya kimwili au kiroho?
Kukosa au kutokuwa na uhai.?
Kutokwa na Roho / Pumzi?
Kukosa au kutokuwa na uhai.?
Kutokwa na Roho / Pumzi?
Ø Ni
hali ya kufarakana au kutengana kwa vitu au hali zinazofanya uhai kuwepo.
Kwakuwa Upo uhai wa aina tatu wa mwilini, nafsini na rohoni; vivyo hivyo na
aina za kifo. Kifo au mauti ni Roho kamili na siyo tukio.
Ø Sisi
sote kwa wakati fulani, labda baada ya kufa rafiki yetu au mpendwa wetu,
tumejisikia kana kwamba tumbo liko tupu, yaani, kuwa na hisia ile ya upweke
inayopita ndani yetu tunapoangalia kwa haraka kuona mwisho wa uhai wa mtu.
Ø "Mavumbi
ya Ardhi" + "Pumzi ya Uhai" = " Roho Hai"
Ø Mwili
Usio na Uhai + Pumzi toka kwa Mungu = Nafsi Hai.
Ø Kila
mmoja wetu anao mwili na akili inayofikiri. Kwa kadiri sisi tunavyoendelea
kuvuta pumzi, tutaendelea kuwa nafsi hai, yaani, roho hai.
Ø Mtu
anapokufa kinyume cha hatua zile za uumbaji zilizoelezwa katika Mwanzo 2:7
hutokea "Nayo MAVUMBI huirudia
ardhi yalikotoka, nayo ROHO [PUMZI YA UHAI] humrudia Mungu aliyeitoa." -
(Mhubiri 12:7).
Kwa sababu kila chenye kimwili
kina cha kiroho chake. Kimsingi uumbaji
ulianzia kwenye ulimwengu wa Roho yaani visivyoonekana viliumba vinavyoonekana
vivyo hivyo kifo kinaanzia ulimwengu wa Roho kuja kwenye ulimwengu wa mwili.
Hebu tutazame kifo kilichotokea
baada ya anguko kwenye hiki kitabu cha mwanzo 2:17
17lakini kamwe usile
matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya, kwa maana siku utakapokula matunda yake,
hakika utakufa.’ Hapa tunakutana na neno linalosema SIKU UTAKAPOKULA , kibinadamu baada ya
kula tu tunda ilibidi hata adamu aanze kuchimba kaburi amzike eva , sasa
alipoona kweli hajafa baada ya kula tunda akahisi Yule nyoka alikuwa sahihi
aliposema “mwanzo 3:4 Lakini nyoka akamwambia mwanamke, “Hakika
hamtakufa.” . hakika eva hakujua kuwa kifo ni Roho na bali ni tukio, ndiyo maana baada ya kula akaona hajafa
akapata ujasiri wa kumpelekea na adam asijue kilichokufa ni ROHO na siyo tukio.
Kama kifo ni tukio basi tusemeje
, je MUNGU alikuwa muongo? Kwamba
watakufa? Majibu yake utaona kuwa kifo
siyo tukio bali ni Roho kamili na ndiyo tunayoita ROHO YA MAUTI IKAIINGIA
DUNIANI baada ya anguko.
2wafalme 2: 21
Kisha akatoka akaenda kwenye
chemchemi na kuitupa ile chumvi ndani yake, akisema, “Hili ndilo asemalo BWANA:
‘Nimeyaponya
maji haya. Kamwe hayatasababisha mauti tena wala kutozaa.’ ” mauti ndo kifo na ndiyo ROHO na siyo tukio na
tazama hapa kwamba ROHO YA MAUTI ipo kwenye maji.
2wafalme 4:40-41
Mchuzi ukagawiwa watu, lakini
walipoanza kula, wakalia, “Ee mtu wa Mungu, kuna mauti ndani ya chungu.”
Nao hawakuweza kula. 41Elisha
akasema, “Leteni unga,” akauweka ndani ya chungu na kusema, “Wagawie watu ili
wale.” Wala hapakuwa na kitu cho chote chenye madhara ndani ya chungu” tazama
hapa kuwa ROHO YA MAUTI IPO SUFURIANI.
Luka 1:79.
………. ili kuwaangazia wale waishio
gizani na katika uvuli wa mauti,
kuiongoza miguu yetu katika njia ya
amani.”………..
Luka 8:
54
……..Yesu
akamshika yule binti mkono na kuita, “Binti, amka!” 55 Roho
yake ikamrudia, naye akainuka mara. Tazama hapa ROHO yake ikamrudia
maana yake uzima wa huyu mtu ni ROHO YAKE.
Marko 14: 4
……Akawaambia,
“Moyo wangu umejawa na huzuni kiasi cha kufa………kumbe moyo
yaani ROHO inaweza ikafa huku mwili wa nyama ungali bado mzima.
Mathew 8: 22
Lakini
Yesu akamwambia, “Nifuate, nawe waache wafu wazike wafu wao.’’ Je kama kifo
ni tukio hawa watazikanaje?
BWANA YESU ASIFIWE ………
GROLY TO GOD , GROLY TO GOD…..
Nimatumaini yangu umeanza kupata
kitu pamoja na kuelewa kile ninachozungumza nawe saa hii.
Ngoja nikupe niliyowahi kukutana
nayo kwenye huduma ya kufunguliwa… siku
moja ambayo nilikuwa nafanya huduma ya kufunguliwa(derivalence), ya mtu
aliyekuwa na mapepo na majini na mizimu na nguvu za kichawi , maombi ya kuvunja
yalipoanza mapepo yalilipuka na kusema huyu tumeshamuua na matanga tumeshafanya
kama wiki mbili hivi zilizopita, na kaburi lake tunalo kwani tulichimba sisi
wenyewe…….
Mengine yakasema unajisumbua tu
kumwombea kwani hawezi kupona tumeshamuua…..
Nilipomaliza huduma anashangaa
kwanza kuwepo yeye kwenye eneo hilo la maombi, lakini pia aka nambia eti
hakumbuki chochote alichokifanya ndani ya siku kadhaa hususani tangu augue
(yaani toka siku ile kwenye ulimwengu wa roho walipomzika basi vivyo hivyo
kimwili akasahau kila kitu), nikamuuliza kama hakumbuki chochote sasa alikuwa
wapi ? akanijibu kwamba alikuwa safarini na wenzake wengi tu ambao hawafahamu. kumbe
unaposhuhudia kuwa leo Fulani amefariki na tunamzika kaburini actually KIROHO
inakuwa ilishatokea zamani sana. Hii haijalishi kwamba hicho kifo ni cha
KIMUNGU AU KISHETANI….Na ndiyo maana watu wengine huota kifo chake kabla ya
kufa.
Hususani pale ambapo binadamu
anatenda tu dhambi basi kwenye ulimwengu wa ROHO mtu huyo anaoonekana ni mfu.(
it looks a dead body) EFESO 2: 1--Kwa habari zenu, mlikuwa wafu katika makosa na
dhambi zenu, …………
Niliwahi kukutana na mtu mmoja ambaye ameokoka na kuanza kusimulia yale
aliyokuwa akifanya kipindi hajaokoka kwani alikuwa mchawi, jambo mmojawapo
alieleza namna ambavyo wanamuua mtu katika ulimwengu wa roho na pia namna ya
kujua kuwa mtu huyu au Yule amekufa kifo cha KIMUNGU AU KISHETANI.
Ukielewa somo hili hakika
hutashangaa unaposikia wafu wanafufuka au wewe mwenyewe kama mtumishi wa MUNGU
unaouweza wa kufufua wafu.
Watumishi wengi sana
tumefanikiwa kuondoa magonjwa kwa uwezo wa JINA LA YESU KRISTO lakini kwenye
kipengele cha kufufua bado tupo nyuma,, kwa sababu nisomapo biblia naona kuwa
popote pale ambapo mtu alikaribia kufa au kufa basi wahusika walitafuta huku na
huku ili kupata watumishi wa MUNGU ili
arejeshe uhai kwa aliyekufa, na hii ilifanyika kabla ya kwenda kuzika….. lakini
hii imekuwa tofauti kwa kizazi cha leo kwani mtu akifa tu basi tunaridhia na
kuishia kuomboleza huku tukisema BWANA
AMETOA BWANA AMETWAA, MUNGU AMPUMZISHE MAHALI PEMA PEPONI, MUNGU AMPE RAHA YA MILELE na maneno kama REST IN PEACE, na mengine
yanayofanana na hayo . kiukweli hii imepelekea hata shetani akaiona fursa ya
kuleta vifo akijua tu kwamba hawa waliobaki watachukulia POA.
Kwa kumalizia niseme hivi : wako
wengi sana binadamu ambao ni DEAD BODY, yaani huyu katika ulimwengu wa
ROHO akina watakatifu wa MUNGU, malaika na jeshi la
mbinguni pamoja na yeye mwenyewe MZEE
WA SIKU yaani MUNGU MWENYE ENZI wanamuona ni dead body is eating, moving,
walking, praying, talking, preaching gospel, studying. Now ask yourself AM I A DEAD OR LIVING BODY?
Wako wengi pia ambao wamekufa
roho zao lakini wanatembea barabarani, wanafanya kazi maofisini, mfano wazinzi,
walevi, wasengenyaji, wachoyo, wachawi, wavaaji mavazi mabaya hawa wote ni DEAD
BODY katika ulimwengu wa ROHO.
Wako ambao pia wameumizwa roho zao
kiasi cha kufa yaani mioyo yao imejaa uchungu(hasira iliyochacha) natamka rasmi
kwamba KRISTO YUKO HAPA KWA AJILI YAKO . maandiko haya yametimia kwenye mioyo
yenu siku ya leo ya kwamba…Wakati mnapokwenda, hubirini mkisema, ‘Ufalme
wa Mbinguni umekaribia.’ 8Ponyeni
wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo wachafu. Mmepata bure,
toeni bure. (Mathew 10:7)
OKOKA KUBALI NA KUMPOKEA YESU
KUANZIA LEO, MKABIDHI MAISH YAKO NA VYOTE VILIVYOKUFA MAISHANI MWAKO VIKIWEMO
NDOA YAKO, KIZAZI CHAKO, FAMILIA YAKO, KAZI YA MIKONO YAKO, WAZAZI NA NDUGU
ZAKO, ELIMU NA AFYA YAKO NA MOYO WAKO HAKIKA YESU KRISTO ATAVIFUFUA NA
UTAONEKANA HAI KATIKA ULIMWENGU WA ROHO NA SIYO DEAD BODY TENA. Kwa maelezo
zaidi nitafute kwa mawasiliano hapo juu na MUNGU kupitia mtumishi wake atakuhuisha.
Asante ROHO MTAKATIFU KWA UAMINIFU
WAKO
Mungu awabariki katika JINA LA YESU KRSITO.
No comments:
Post a Comment